Kundi la watoto wenye ulemavu wa ngozi nchini Tanzania ambao mikono na miguu yao ilikatwa na waganga wachawi wamerudi kutoka Marekani wakiwa na viungo bandia.

Mwigulu Matonange Magesa (kushoto) na Baraka Cosmas Lusambo wakisaidiana kuwekana viungo katika Hospitali ya watoto ya Shriners
Watoto watano walisafirishwa hadi Hospitali ya Watoto ya Shriners iliyopo Philadelphia mwezi Juni kwa ajili ya matibabu ya majeraha ya kikatili waliyoyapata na hivyo kuwekewa viungo bandia.

Kabula Nkarango Masanja, 17, akifuta machozi wakati wa kuagana na muasisi wa GMRF Elissa Montanti katika uwanja wa ndege wa JFK, New York
Wa kwanza kati yao ni Kabula Nkarango Masanja, 17, amerudi nchini Tanzani, na kuwaambia madaktari wa Marekani na wafanyakazi jamii wa Tanzania kuwa: “Mungu awe nanyi”.
Walemavu wa ngozi wanafanyiwa ukatili nchini Tanzania na waganga ambao wanaamini viungo vyao vinaleta utajiri na bahati.

Mwigulu Matonange Magesa (kushoto) na Baraka Cosmas Lusambo wakisaidiana kuwekana viungo katika Hospitali ya watoto ya Shriners
Kila mwaka mlemavu wa ngozi hutekwa na kukatwa viungo vyake, nywele zake, meno na hata nyeti zake hukatwa na mapanga ili kutumika kuleta bahati na kuuzwa kwa bei aghali.

Monica Watson (kushoto) kutoka Global Medical Relief Fund, Ester Rwela kutoka Under The Same Sun, pamoja na mtalaamu Amanda Wodzinski (kulia) wakimsaidia Mwigulu Matonange Magesa kuweka kiungo chake
Montanti, ambaye anaishi karibu na nyumba ya hisani ya “Dare to Dream”, ametumia miaka mingi kusafirisha watoto waliopoteza viungo kutoka maeneo mengi yenye ukatili huo yakiwemo Bosnia, Haiti, Iraq, Afghanistan, Libya na Syria.


Post a Comment Blogger Facebook